HEPATITIS B
Ugonjwa wa Homa ya ini(Hepatitis B) unaaminika kuwa hatari zaidi kuliko hata UKIMWI.
HOMA YA INI (HEPATITIS B)
Homa ya Ini ni ugonjwa unaoambukizwa kwa njia ya virusi ambavyo vikishaingia mwilini hushambulia ini kabla ya kugeuka maradhi sugu. Virusi hivyo vinaitwa HBV(Hepatitis B Virus).
Virusi hivyo husambazwa kwa njia ya damu au majimaji mengine ya mwilini, mfano mate au jasho. Inakadiriwa takribani watu 600,000 wanapoteza maisha Duniani kote kutokana na ugonjwa wa Homa ya Ini kila mwaka.
Ugonjwa huu kama haujatibiwa hutengeneza uvimbe katika ini na kusababisha kansa ya ini na baadaye kifo.
MAAMBUKIZI.
Kama ilivyo kwa UKIMWI, virusi vya homa ya Ini huambukizwa kwa njia ya kujamiiana, mate, jasho na mwingiliano wowote ule wa damu. Lakini pia HBV husambazwa kutoka kwa mama kwenda kwamtoto wakati wa kuzaliwa.
NA HIZI NDIO NJIA KUU ZA MAAMBUKIZI YA HOMA YA INI (HEPATITIS B)
1.Kujamiana bila kinga
2.Kunyonyana ndimi
3.Mama kwenda kwa motto wakati wa kujifungua
4.Kuchangia vitu vya ncha kali kama sindano n.k
5.Kuchangia miswaki
6.Kuchangia taulo na mwenye ugonjwa huo
7.Kuchangia damu isiyo salama
8.Kubadilishana nguo au kukumbatiana wakati mkiwa mnavuja jasho
TAFITI ZA KITAALAMU ZINAONYESHA KUWA VIRUSI HIVYO NI HATARI KULIKO HATA VYA UKIMWI,
UNAJUA KWANINI?
UNAJUA KWANINI?
Virusi hivi vina uwezo wa kuishi nje ya mwili wa binadamu(yaani nje ya mfumo wa damu mpaka siku saba).
Virusi vya UKIMWI(VVU) havina uwezo wa kuishi nje ya mfumo wa damu hata kwa dakika moja.
Tafsiri yake ni kwamba kama kirusi kipo kwenye ngozi kitaendelea kuwa hai kwa siku saba na katika kipindi hicho mtu anaweza kuambukizwa kwa njia ya damu au jasho.
Kwa wastani kirusi cha HBV kikishaingia mwilini, hupevuka ndani ya siku 75, hata hivyo upo uwezekano wa kupevuka kati ya siku 30 hadi 180.
Ndani ya siku 30 mpaka siku 60, mtu mwenye HBVanaweza kugundulika ikiwa atapimwa.
Mtu mwenye Homa ya Ini ana wastani mdogo wa kuishi kuliko mwenye UKIMWI.
DALILI ZA UGONJWA WA HOMA YA INI (HEPATITIS B)
Watu wengi hawaonyeshi dalili yoyote. Kwa maana hiyo mtu anaweza kuishi na HBV na kusababisha maambukizi kwa wengine bila kugundulika.
Hata hivyo watu wengine husumbuliwa na homa kali na dalili ambazo hudumu kwa wiki kadhaa.
Dalili hizo ni,
1.Uchovu
2.Kichefuchefu
3.Mwili kuwa dhaifu
4.Homa kali
5.Kupoteza hamu ya kula
6.Kupungua usito
7.Maumivu makali ya tumbo upande wa kulia
8.Macho na ngozi kuwa vya njano
9.Mkojo mweusiKwa wagonjwa wengine,
Pia fahamu virusi vya Hepatitis B hukua hadi kusababisha ini kuharibika kabisa. Hali hii huitwa saratani ya Ini.
TIBA
Mpaka sasa homa ya Ini haina tiba, lakini habari njema ni kwamba kuna chanjo.
NB : Ugonjwa huu ukishafika hatua ya ini kuharibika (Saratani ya ini) maana yake kinachofuata ni kifo.
Pamoja na kutokuwepo tiba, kuna chanjo ambayo iwapo ukiipata itakuepusha na maambukizi.
Chanjo za ugonjwa huu hutolewa hospitali kote nchini na hutolewa mara tatu.
Kwa ambae hajaambukizwa chanjo humuepusha kabisa na ugonjwa huu. Hivyo ni muhimu sana.
Kwa aliyeambukizwa chanjo humsaidia kuisha zaidi ya miaka 20, hivyo ni muhimu sana kupata chanjo.
Asilimia 30-50 ya watoto chini ya miaka 6, Hepatitis B hukua mpaka kuwa sugu na baadaye nikifo.
Asilimia 90 ya watu wazima wanaopata HBV, virusi hivyohutoweka ndani ya miezi sita. Yaani uimara wa ini husababisha virusi kupotea.
TIBA
Mpaka sasa homa ya Ini haina tiba, lakini habari njema ni kwamba kuna chanjo.
NB : Ugonjwa huu ukishafika hatua ya ini kuharibika (Saratani ya ini) maana yake kinachofuata ni kifo.
Pamoja na kutokuwepo tiba, kuna chanjo ambayo iwapo ukiipata itakuepusha na maambukizi.
Chanjo za ugonjwa huu hutolewa hospitali kote nchini na hutolewa mara tatu.
Kwa ambae hajaambukizwa chanjo humuepusha kabisa na ugonjwa huu. Hivyo ni muhimu sana.
Kwa aliyeambukizwa chanjo humsaidia kuisha zaidi ya miaka 20, hivyo ni muhimu sana kupata chanjo.
Asilimia 30-50 ya watoto chini ya miaka 6, Hepatitis B hukua mpaka kuwa sugu na baadaye nikifo.
Asilimia 90 ya watu wazima wanaopata HBV, virusi hivyohutoweka ndani ya miezi sita. Yaani uimara wa ini husababisha virusi kupotea.

